Karibu ABlinkA

Home of innovations

Rejea Edeni

Nyumba ya Ubunifu, Afya na Ustawi

ulimwenguni kuna nini?

KUHUSU SISI

Dhamira yetu ni kuhamasisha, kuratibu, kufundisha na kusaidia vijana na wanawake katika jamii kutumia fursa zilizopo kubuni bidhaa na huduma zenye ubora wa juu, zinazotatua changamoto za kijamii, kutengeneza ajira, na kuinua vipato kwa kujiajiri na kuajiri wengine.

KUHUSU SISI

Dhamira yetu ni kuhamasisha, kuratibu, kufundisha na kusaidia vijana na wanawake katika jamii kutumia fursa zilizopo kubuni bidhaa na huduma zenye ubora wa juu, zinazotatua changamoto za kijamii, kutengeneza ajira, na kuinua vipato kwa kujiajiri na kuajiri wengine.

Miradi

Ufugaji wa Kuku na Samaki

Tunatoa mafunzo kuhusu ufugaji wa kuku na samaki kwa njia za kisasa zinazohakikisha uzalishaji bora na faida kubwa. Wageni wanajifunza kuhusu uchaguzi wa mbegu bora, ulishaji, udhibiti wa magonjwa, na mbinu...

Kilimo cha Matunda na Mboga

Tunalenga kuzalisha matunda na mboga zenye thamani kubwa sokoni, hasa mijini kama Morogoro. Wanaoshiriki wanajifunza kuhusu uchaguzi wa mazao, matumizi ya mbolea asilia, umwagiliaji...

Usindikaji wa Bidhaa na Elimu kwa Jamii

Tunatoa mafunzo ya usindikaji wa mazao ili kuongeza thamani na kupanua soko. Hii inahusisha usindikaji wa bidhaa za shamba, kutengeneza bidhaa za afya ya ngozi kama sabuni na mafuta ya asili...

Huduma Zetu

Karibu ABLINKA, mahali ambapo huduma zinakutana na ubora wa hali ya juu ili kukupa uzoefu wa kipekee. Tunajivunia kukuletea huduma mbalimbali zinazokidhi mahitaji yako kwa viwango vya juu, mazingira tulivu, na huduma za kibinafsi.

Malazi

Tunatoa malazi ya kifahari kupitia mfumo wa Bed & Breakfast (B&B). Vyumba vyetu ni safi, vya kisasa, na vinakupa utulivu wa hali ya juu.

Ubunifu

Furahia vyakula vya asili vilivyoandaliwa kwa viwango bora, pamoja na matunda freshi kutoka shambani. Pia, tunatoa vinywaji vya asili kwa afya bora

Kumbi

Tunakodisha kumbi ndogo na za kati kwa mikutano, semina, na sherehe. Mazingira yetu ni tulivu na yanafaa kwa kila tukio lako maalum

Afya na Mazoezi

Tunatoa mazoezi, massage, na tiba asilia kwa afya njema. Programu zetu zinakuwezesha kujenga mwili wenye nguvu na kupunguza msongo wa mawazo

CEO

Dkt. Bunini Manyilizu ni Daktari wa Tiba ya Binadamu aliyehitimu Chuo Kikuu cha Muhimbili, mwenye Shahada ya Uzamili katika Afya ya Jamii na Shahada ya Uzamivu katika Usalama wa Afya dhidi ya Sumu. Ni mkufunzi, mtafiti na mwandishi anayejulikana kwa uwezo wake wa kufafanua masuala ya kisayansi kwa lugha rahisi. Akiwa mshauri aliyethibitishwa na SIDO, amejikita katika kuwawezesha wajasiriamali kupitia usindikaji wa bidhaa za lishe, urembo na utanashati.
Pia anahudumu katika Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), ambako anashughulika na Tafiti, Ubunifu na Maendeleo ya Kisayansi. Ana mtandao mpana wa wanasayansi, watafiti na wabunifu ndani na nje ya Tanzania. Dkt. Bunini ni Mwanzilishi wa ABlinkA Trust iliyoko Morogoro, inayolenga kuhamasisha jamii katika kujitegemea, kuboresha maarifa ya Afya-Kinga, Kilimo, Ufugaji, Usindikaji wa bidhaa, na matumizi ya Teknolojia na Ubunifu kwa ustawi wa jamii.

Business

Startup, Management, Marketing, and Sales

Research

Concept proposal, Data Entry, Report Editing Services

Book writing and publication

Teaching and learning methods are applied) accordingly

Creativity and Innovativeness

Concepts of innovation and innovation, Exposure and practical

Tunaweza kukuunganisha kila mahali

Tunakuunganisha na wataalamu, taasisi, teknolojia nafuu, ubunifu na fursa ili kukusaidia kufikia malengo yako ya ujasiriamali na ajira.

Tunaweza kukuunganisha kila mahali

Tunakuunganisha na wataalamu, taasisi, teknolojia nafuu, ubunifu na fursa ili kukusaidia kufikia malengo yako ya ujasiriamali na ajira.

WASILIANA NASI

Namba ya simu

 +255780944260

Email

ablinka2025@gmail.com

Makazi

Tanzania, Morogoro Municipal 

Mitandao ya Kijamii

Tuma Ujumbe


]